Wednesday, August 3, 2016

Ugonjwa wa Mgongo Wazi na Tiba Yake


Mgongo wazi au kwa jina la kitaalam huitwa ‘spina bifida’, ni ugonjwa au hali ambayo mtoto anazaliwa nayo huku uti wa mgongo ( ule mshipa wa fahamu mkubwa unaotoka kwenye ubongo) ukiwa wazi, kutokana na mifupa ( vipingili vya uti wa mgongo) kutokufunga vizuri.

Kwa kawaida mara tu baada ya mimba kutunga uti wa mgongo hutengewa nusu upande mwingine na nusu upande mwingine.

Baada ya hapo nusu ya mkono wa kulia huunganiswa na nusu ya mkono wa kushoto kama vile mtu anayefunga zip ya nguo.

Ni wakati wa muunganiko huo ndio kasoro inaweza itokee na hivyo sehumu fulani ikawa haijaziba, kama vile ambayo zip ikiharibika inaweza iache katundu mahali.

Sababu zinazofanya kasoro hiyo itokee ni kama kupigwa X ray mama mja mzito, matumizi ya dawa za kifafa, upungufu wa ‘folic acid’, na maambukizi ya baadhi ya virus kwa mama mjamzito.

Shida hii inaweza ikatokea peke yake au pamoja na ‘hydrocephalus’ yaani ugonjwa wa kichwa kikubwa.

Mara nyingi hutokea peke yake lakini baadae ile sehemu iliyowazi hupitisha mambukizi na kusababisha ‘meningitis’, ambayo hushambulia ule utando unaofyonza ‘Cerebral Spina Fluid’ na hivyo kufanya maji yaanze kurundikana kwenye kichwa.
Spina bifida huwapata watoto 3 kila watoto 10000 wanaozaliwa.

Fika leo Afya Bora Herbal Clinic, ili uweze pata matibabu ya tatizo hili na mengine kadhaa wa kadhaa.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI YAKO

Name

Email *

Message *