Showing posts with label MAJANGA HOSPITALINI. Show all posts
Showing posts with label MAJANGA HOSPITALINI. Show all posts

Tuesday, August 2, 2016


Msichana aliyefahamika kwa jina la Jésica Santillán, aliwasili katika hospitali ya Duke University Medical Center Marekani, kutokea nchini Mexico ili kupata matibabu kufuatia kuwa na matatizo ya moyo na mapafu.

Jésica alikuwa ni msichana wa umri wa miaka 17, raia wa Mexico, pengine alikuwa na ndoto nyingi kwa taifa lake na familia kwa ujumla lakini alifariki dunia muda mfupi mara baada ya kufanyiwa upasuaji.

Sababu ya kifo chake ilitokana na kuhamishiwa moyo na mapafu (heart-lung transplant) kutoka kwa mtu ambaye hafanani naye kundi la damu.

Je, ulishawahi kupatwa na tatizo kama hilo au linalofanana na hilo? Tuambie kupitia kisanduku cha maoni au tuandikie barua pepe kupitia afyaboraherbalclinic@gmail.com
0


Huko nchini Marekani katika mji wa Commack, New York, mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Nancy Andrew alipata ujauzito usiotokana na mbegu za mumewe baada ya kupandikizwa mbegu za mwanaume mwengine katika kliniki ya upandikizaji (New York Fertility Clinic).

Yeye na mume wake walitegemea kuongezeka kwa mtoto katika familia yao. Walichokuwa hawatarajii ni kupata mtoto mweusi kuliko wazazi wake.

Vipimo vya kutambua vinasaba (DNA Test) vilionesha kuwa madaktari katika kliniki ile walipandikiza mbegu za mwanaume mwengine kwenye mayai ya Nancy Andrew.

Wapenzi hao mpaka sasa wanamlea mtoto huyo waliyempa jina la Jessica kama wa kwao. Hata hivyo, wawili hao wanaona hawakutendewa haki na mwenye kiliniki hiyo pamoja na daktari aliyechanganya mbegu hizo.

Je, ulishawahi kupata majanga yoyoote hospitalini? Tuambie kupitia kisanduku cha maoni au tutumie barua pepe kupitia afyaboraherbalclinic@gmail.com
1

ANDIKA MAONI YAKO

Name

Email *

Message *