Saturday, August 6, 2016

Hili Ndio Suluhisho La Degedege


Degedege Ni Nini?

Ni hali ya ghafla ya kutingishika kwa mwili mzima au miguu na mikono, ambayo husababishwa na kukakamaa kwa misuli ya mwili. 

Hali hii uhusishwa na magonjwa ya ubongo kama kifafa, vichocheo vya kwenye damu kama upungufu wa sukari(hypoglycemia), upungufu wa oxygen(hypoxia), kushuka kwa shinikizo la damu(hypotension) na maambukizi na homa ya degedege.

Homa ni Nini?

Ni hali ya kawaida ya mwili kujikinga na maambukizi. Na kwa watoto hutokea pale joto la mwili linapokuwa zaidi ya nyuzi 38 za sentigredi.


Homa ya Degedege Ni Nini?

Ni degedege linalotokea kwa watoto ghafla likiambatana na homa kali iliyotokana na kuongezeka haraka kwa joto la mwili. Ugonjwa huu utokea kwa wastani wa asilimia nne (4%) ya watoto walio kati ya umri wa miezi sita na miaka mitano. 

Watoto wengi ambao hupatwa na ugonjwa huu huwa haiwapelekei baadae kuwa na matatizo ya kudumu kama kupata ugonjwa wa kifafa, niasilimia tatu (3%) tu ambao wanaweza baadae kupata ugonjwa wa kifafa.

Mmoja kati ya watoto watatu anbao wamewahi kuwa na homa ya degedege wanaweza wakapatwa tena na tatizo hili.baabhi ya watoto wanaweza wasipatwe kabisa na tatizo hili au wakapatwa mara moja tu kwa maisha yao yote. Lakini hauna jinsi ya kutabiri ni mtoto yupi ambaye anaweza kupatwa na shambulio hili.


Homa ya Degedege Hutokea kwa Watoto Gani?


Watoto wanaweza kurithi tabia hii ya kuumwa homa ya degedege kutoka kwa wazazi wao. Kama mama au baba aliwahi kuumwa ugonjwa huu basi mtoto ana asilimia 10-20 zaidi ya kuumwa ugonjwa huu hukilinganisha na yule ambaye wazazi wake hawakuwai kuumwa ugonjwa huu.

Homa isababishwayo na maabukizi yoyote yale kama virus, bakteria na parasite

Dalili za Homa ya Degedege ni Zipi?

Shambulio la ugonjwa huu likijitokeza mtototo uanza na kupotewa na fahamu na muda mfupi baadae mwili, miguu na mikono uanza kukakamaa na kurudisha kichwa nyuma, baada ya hayo miguu na mikono uanza kujitikisa.

Kushindwa kupumua na kutokwa na mapovu mdomoni

Macho kugeukia nyuma na kuonekana kwa sehemu nyeupe ya jicho

Shambulio huisha baada ya muda mfupi mara nyingi chini ya dakika tano
 
Baada ya shambulio mtoto hupitiwa na usingizi mzito kama takribani dakika 30 hadi saa nzima.

Akizinduka anaweza kushindwa hata kukutambua na akawa atamani kitu chochote kwa muda huo.
 
Nini cha Kufanya Mtoto anapopatwa na Shambulio?

Tulia na usichanganyikiwe

Ondoa vitu vya hatari karibu na mtoto na muweke sehemu ya usalama kama sakafuni.

Usijaribu kuweka kitu chochote mdomoni kwa mtoto hata vidole vyako.


Angalia muda wa shambulio kuanza hadi litakapo isha ili umueleze daktari.


Baada ya shambulio kuisha mlaze mtoto kwa upande na usimuamshe muache apumzike.
Shambulio la homa ya degedege sio kifafa na mtoto hapati maumivu yoyote wakati wa shambulio kwa hiyo usimpe dawa yoyote ile.


Baada ya hayo mpeleke mtoto kwenye zahanati, kituo cha afya au hospitali ya karibu kwa matibabu zaidi ya mtoto.



Fika Leo Afya Bora Herba Clinic iliyopo Njia panda ya Kigogo Karibu na Roundabout Kupata Tiba ya Tatizo hili na mengine mengi.

4 comments:

  1. Mimi ninaswali Nina mtoto ambaye homa humtokea awamu tatu katika mwezi

    ReplyDelete
  2. Mim mwanangu insjirudia kwa nini

    ReplyDelete
  3. Msaada ndugu zangu mwanangu ana miez mitatu kachanga kuna muda anakakamaa mwili mzma na kulia na anastuka sana wakati amelala jamani shida nini na nifanyaje wakati mwingine ucku anastuka analia sana

    ReplyDelete

ANDIKA MAONI YAKO

Name

Email *

Message *