Saturday, August 6, 2016

Tiba Ya Kujikojolea Kitandani Ipo


Nini maana kukojoa kitandani?

Hii ni hali ya kukojoa kitandani wakati mtu amelala, tatizo hili linapotokea kwa mtoto wa chini ya miaka sita sio ugonjwa na mara nyingi huisha lenyewe.

Watoto wengine huendelea kukojoa kitandani mpaka umri wa kubalehe na kuvunja ungo. Lakini tatizo hili hupotea anapokua mtu mzima kabisa.

Sababu kwanini mtoto anayeweza kukojoa mwenyewe mchana kuendelea kukojoa wakati amesinzia haileweki , mara nyingi watoto wa kiume hujikojolea sana kuliko wa kike lakini kuna mahusiano ya kurithi tatizo hili yaani kuna uwezekano mkubwa baba wa mtoto au mama alikuaga kikojozi pia kwenye utoto wake.

Kwa watu wazima tatizo la kukojoa kitandani hua ni ugonjwa flani. Mfano wa magonjwa haya ni,

Kisukari (diabetes mellitus):

Ugonjwa huu huambatana na dalili ya kupata kiu sana, njaa kali na kwenda kukojoa mara kwa mara wakati wa usiku.

Magonjwa ya njia ya mkojo (chronic urinary tract infection):
Hii ni kutokana na kuharibika kwa kibofu cha mkojo ambacho ni muhimu katika kutambua ujazo wa flani wa mkojo ili mtu aende kukojoa hivyo kuugua kwa kibofu husababisha kisifanye kazi vizuri. mfano cystitis

Magonjwa au kuumia kwa mishipa ya fahamu ( structural or infections of nerves):

Mishipa ya fahamu ni muhimu katika kutoa taarifa za ujazo wa mkojo kwenye kibofu. Kibofu kinapofikisha ujazo wa 300mils mpaka 400mils taarifa hutumwa kwenye ubongo, kisha ubongo hurudisha taarifa za kuruhusu mtu akojoe.

Kuharibika kwa mishipa hii ya fahamu husababisha kujikojolea mfano kuvunjika kiuno, kiharusi, magojwa ya akili, multiple sclerosis na alzeheimers disease.

Kuvimba kwa tezi dume (prostate enlargement):

Tezi dume ni kiungo kinachopitiwa katikati na mirija ya mkojo{urethra}, hivyo kuvimba kwake hubana mirija hiyo na kusababisha kukojoa mara kwa mara[incontinence}.

Vipimo ambavyo hupimwa mahospitalini:

Kupima mkojo kuangalia kama kuna shida yeyote ya mfumo huo.

Kupima puru kama tezi dume imevimba.{digital rectal examination}

X-ray kuangalia kama kuna tatizo la umbo la kibofu cha mkojo.

Kama Unasumbuliwa Na Tatizo Hili Fika Leo Afya Bora Herbal Clinic Iliyopo Njia Panda Ya Kigogo, Karibu na Roundabout kupata tiba na tatizo kutojirudia tena.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI YAKO

Name

Email *

Message *