Recent Post

Wednesday, August 10, 2016


Tabia ya mtu inatokana na malezi aliyoyapata kwa kiasi kikubwa toka kwa wazazi,pia toka kwa walimu mashuleni, mafundisho ya dini,na toka kwa watu anaoonana nao na kuchangamana nao kila siku za maisha yake hasa wakati wa umri mdogo. Kulea watoto kulingana na tamaduni zetu katika karne hii ya teknolojia ni changamoto kubwa.

Watoto wa Dijitali ni wale ambao wamezaliwa katika karne hii ambayo teknolojia ya habari na mawasiliano imesomnga mbele sana kiasi ambacho taarifa zimekuwa nyingi kupita uwezo wakuzidadavua. Wazungu wanaita “Information Overload“.

Watoto hawa wa dijitali wanafahamu mambo mengi sana kuliko ambavyo wanatakiwa kufahamu katika umri husika jambo ambalo linaleta changamoto kubwa katika kulea watoto kwa wazazi wa zamani ambao walizaliwa kipindi ambapo teknolojia haikuwa katika kiwango hiki na mfumo wa malezi walioupata unatofautiana sana na wa sasa na pengine haufanyi kazi katika mazingira ya kisasa. Wazazi hawa nimewaita “Wazazi wa Analojia”.

Katika hali hii utakuta mtoto anafahamu mambo mengi tu ambayo wazazi hawayajui,ina maana mzazi anajifunza toka kwa mtoto,hii ina maana gani? Kuna madhara mara mbili

  • Mzazi anakosa kujiamini katika jukumu lake la kumfundisha mtoto kwani anatambua sasa kuwa mtoto ni mjuaji wakati ungine kumzidi,na anaweza kuamua kutofanya hilo jukumu kwa kujua mtoto anafahamu tayari. Wakati mwingine inakuwa si sahihi.

  • Mtoto anatambua baada ya muda kuwa mzazi wake hafahamu mambo mengi na kuwa yeye anafahamu zaidi. Hivyo naye anaacha kuuliza au kutaka kufahamu toka kwa wazazi. Hivyo anaweza akafanya vitu kwa ufahamu wake tu binafsi au kwa kutafuta msaada sehemu nyingine nje na wazazi wake. Na huenda msaada atakao pata ukawa sio sahihi.

Hali hii ni hatari katika ulezi wa watoto katika jamii yetu na ni lazima kuliangalia kwa mapana sana na kuchukua hatua stahiki.



0


Ugomvi baina ya wapenzi katika mahusiano ni kitu cha kawaida kutokana na watu hao wawili kutoka katika malezi na mazingira tofauti ya ukuaji toka wakiwa wadogo hadi watu wazima.

Wawili hao wanapoaanza kujenga mahusiano na kukaa pamoja kama familia,kuna vitu kadhaa ambavyo kila mmoja wao huvitazama tofauti na hivyo kuleta migongano. Migongano ambayo inaweza ikarekebishika kama wenza hao watamua kuifanyia kazi na kuelewana.

Kuna vitu vingi ambavyo husababisha ugomvi na migongano ndani ya mahusiano ya mke na mme na hapa tunaeleza sababu kuu ambazo kwa kawaida hutokea karibu katika kila mahususiano

1. Wivu Na Kukosa Kujiamini

Wivu unatokana na jinsi ambavyo mpenzi mmoja anavyohusiana na watu wengine wa jinsia tofauti. Inaweza ikawa marafiki,wafanyakazi wenza au wapenzi wa zamani. Vyovyote vile itakavyokuwa ni kwamba wivu unasababisha ugomvi katika mahusiano mengi.

Kunatakiwa kuweka mipaka ya kutosha na iliyo wazi ili kujenga uaminifu kwa mpenzi wako na kumpa kujiamini. Mpenzi ambaye hajiamini ni tatizo kubwa kwani uwezekano wa kuanzisha ugomvi ni mkubwa.Hivyo ni vizuri ukamjengea mweza wako katika mapenzi kujiamini kwa kuwa mwaminifu.

Uaminifu ni kitu kimoja kikubwa sana katika mapenzi. Kama mwenza wako akikuamini hakutakuwa na wivu wa kupita kiasi na pia atakuwa anajiamini kuwa yeye peke yake ndio chaguo lako na hakuna mwingine.

2. Mawasiliano Finyu

Mawasiliano yanapovunjika katika mahusiano ugomvi ni kitu cha kawaida kutokea.

Mawasiliano ya kawaida kati ya wapenzi husaidia sana kutoa wasiwasi wa nyendo za mwenza wako. Huleta amani na kujenga uaminifu kwa mpenzi kwako.

Kuzungumza juu ya mipango yako ya mendeleo kama ujenzi au biashara ni vitu ambavyo ni muhimu sana kuvifanya vinginevyo utajenga wasiwasi kwa mweza wako na itasababisha ugomvi wa mara kwa mara.

Kuwa muwazi kwa mipango ya maendeleo binafsi,ya familia yako na ndugu.

Utafiti unaonyesha kuwa wapenzi wanaoongea na kusikilizana mara kwa mara hawagombani mara nyingi kama wale wasio na mawasiliano ya kutosha.

3. Masuala Ya Fedha

Japokuwa fedha si msingi wa mapenzi,lakini ni kitu ambacho kinahitajika sana katika maisha ya kila siku ya kila mtu na ya familia. Na kimekuwa ni mojawapo ya vitu ambavyo wapenzi katika mahusiano au ndoa hugombana sana juu yake.

Mwenza mmoja anapokuwa mtumiaji mbaya wa fedha na mwingine siyo,huibua malalamiko na ugomvi. Baadhi ya wapenzi hasa wanawake hawataki kuchangia kwa kiasi kikubwa katika mahitaji ya msingi ya nyumbani na badala yake kuwaachia mzigo mkubwa wanaume.

Hili linaibua malalamiko mengi kwa baadhi ya wanaume,na wakati ungine toka kwa wanawake. Matumizi makubwa ya fedha kwaajili ya pombe na sharehe nyingine kwa wanaume na baadhi ya wanawake kumekuwa mojawapo ya sababu za ugomvi juu ya fedha katika mahusiano.

Ni muhimu kwa wenza wawili kupanga jinsi ambavyo fedha zao zitapatikana na kutumika. Vipaumbele vya kufanyika kwanza na kiasi cha kutumika kwajili ya starehe na urembo kwa wanawake kwa mfano.

4. Masuala Ya Familia

Familia ya nani ianze kwanza na ipi ifuate ni tatizo kubwa katika mahusiano. Upendeleo wa upande mmoja ambao kwa asili huwa unatokea tu ni chanzo cha ugomvi ndani ya nyumba.

Mitazamo tofauti kati ya mmojawapo katika wapenzi na familia ya mwenza wake husababisha kutoelewana kwa wapenzi hao ndani ya nyumba.

Mbaya sana inakuja pale wanandugu wanapoingilia mambo ya ndani ya nyumba yenu. Wazazi wa kike na mawifi mfano, wamejulikana kusababisha matatizo mengi kwenye familia za watoto na kaka zao.

Kuepukana na hili ni muhimu kwa wapenzi ndani ya nyumba kuweka mipaka kwa ndugu ambayo haitaathiri uhusiano nao kama ndugu.

Pia ni muhimu kwa wenza hao kuweka mikakati ya pamoja juu ya kuhusiana nakusaidia ndugu toka katika familia zao mbili.

5. Suala La Unyumba

Japo kuwa suala kufanya mapenzi si kila kitu kwa wapenzi ndani ya nyumba lakini linachangia sana katika kuleta ugomvi aina yao. Kufanya mapenzi kupita kiasi au mara chache kunaleta matatizo kwa wapenzi hasa ambao wana uhitaji tofauti.

Wengine wanaona kama mpenzi ambaye hahitaji kufanya mapenzi mara nyingi na mwenzake labda anauhusiano na mtu mwingine zaidi yake. Au hamvutii tena kama zamani na huenda akaanza kuangalia nje.

Hii inajenga kutojiamini na kupoteza uaminifu,ambalo ni tatizo jingine kubwa katika mahusiano kama tulivyoonesha mwanzoni.

6. Vipaumbele Katika Maisha

Wapenzi wawili wanapokuwa na mipango na malengo tofauti ni tatizo kubwa. Watu wanapokuwa katika uhusiano ambao ni wa kuishi daima,malengo na vipaumbele vyao ni lazima vioanishwe na juhudi za kila mmoja zilenge katika kufanikisha mipango hiyo ya pamoja.

Kunapotokea kuwa kila mmoja ana malengo tofauti basi hata vipaumbele vitakuwa tofauti na hapo ndipo shida zinapoanzia.

7. Uaminifu

Uaminifu katika mahusiaono ni jambo la muhimu sana. Bila uaminifu ni ngumu sana kwa mahusiano yoyote kudumu.

Uaminifu ni kitu ambacho hujengwa kwa muda mrefu na kikipotea ni ngumu sana kukirudisha. Japo inawezekana kujenga upya uaminifu lakini huchukua muda mrefu sana.

8. Wapenzi,Marafiki Na Maisha Ya Zamani

Mojawapo ya vyanzo vya ugomvi kati ya wapenzi ni wapenzi wa zamani. Mawasiliano ya aina yoyote na wapenzi wa zamani huleta wasiwasi mkubwa kwa mpenzi wa sasa. Ni kitu ambacho wapenzi wawili wanahitaji kuongea na kupanga jinsi ya kuepukana na matatizo ambayo yanaweza kusababishwa na historia zao za maisha.

Kuepukana na hii ni vyema kuvunya uhusiano wa aina yoyote na wapenzi wa zamani labda tu kama wapenzi hao ni wazazi wenza au mnafanya kazi pamoja na ni ngumu kutokuonana au kuwasiliana.

Suala linalofanana na hili ni uhusiano na baadhi ya marafiki wa jinsia moja ambao wanachukuliwa kuwa mfano mbaya na mpenzi wako. Kama haiwezekani kutowasiliana na kuonana na wapenzi wa zamani au marafiki, basi ni vyema wakawa marafiki wa familia nzima na mawasiliano yoyote kati yenu nao yawe wazi pasipo kificho.

9. Watoto

Suala la uleaji na ukuzaji wa watoto linasababisha ugomvi mara nyingi kati ya wazazi. Jinsi gani mtoto avae au shule ipi aende linapelekea wazazi wengi kugombana.

Ni jambo la muhimu sana kukubaliana juu ya mambo ya msingi juu ya malezi ya watoto. Tofauti za wazazi ziangaliwe kwanza vinginevyo zitaingilia malezi ya watoto na kusababisha ugomvi juu yao.

10. Kazi Za Nyumbani

Imekuwa kama utamaduni kwa waafrika kuacha kazi nyingi kama si zote za nyumbani kwa mke. Kwa Wanawake ambao wanafanya kazi pia inakuwa ngumu sana. Hili linasababisha pia ugomvi kwa wapenzi nyumbani. Kama nguo ambazo mume anazivaa na kuzichafua tu bila ya kujali kuwa mweza wake ataumia wakati wa usafi na ikiwa yeye mwenyewe hajishughulishi na kufanya baadhi ya kazi za nyumbani ni wazi itasababisha ugomvi.

Ni vyema wanaume kuchukua baadhi ya majukumu nyumbani hata kama kutengeneza bustani au kulisha chakula mifugo.

0

Tuesday, August 9, 2016


Ugonjwa wa kaswende ni ugonjwa wa zinaa unaosababishwa na bakteria aina ya ‘Treponema pallidum’.

Ugonjwa huu ni kati ya magonjwa ya zinaa yanayoongoza kwa kusababisha madhara mengi.

Maambukizi ya kaswende wakati wa ujauzito huleta madhara mengi sana kama vile kujifungua kiumbe ambacho kimeshakufa, mtoto kuathirika na ugonjwa huu wakati wa kuzaliwa, mtoto kupata matatizo wakati wa ukuaji wake, degedege na kuongezeka kwa vifo vya watoto wachanga.

Ugonjwa wa kaswende huathiri zaidi ya mimba milioni moja duniani kote kila mwaka na kuchangia theluthi mbili ya vifo vya watoto wanaozaliwa wakiwa tayari wameshakufa katika nchi za maeneo ya chini ya Jangwa la Sahara.

Asilimia 30 ya mimba zinazoathiriwa na kaswende huishia watoto kufariki wakati wa kuzaliwa.

Pia asilimia nyingine 30 ya mimba zinazoathiriwa na kaswende husababisha watoto wanaozaliwa na ugonjwa huu kupata matatizo ya ukuaji, degedege na kuongezeka vifo vya watoto kwa asilimia 50. Kwa mfano,

Taasisi ya kudhibiti Ugonjwa wa UKIMWI nchini Tanzania (Tanzania National AIDS Control Programme) au NACP katika ripoti yake ya utafiti uliofanywa chini ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii nchini ilitangaza kuwa, maambukizi yote ya kaswende wakati wa ujauzito Tanzania bara kati ya mwaka 2003 hadi 2004 yaliongezeka kwa wastani wa asilimia 6.7 kwa ujumla, kuanzia mkoani Kilimanjaro ambako maambukizi yalikuwa ya asilimia 0.4 hadi mkoani Tabora ambako yalikuwa ya asilimia 32.

Magonjwa ya UKIMWI na kaswende mara nyingi huambatana pamoja ambapo pia ugonjwa wa zinaa wa kaswende huongeza uwezekano wa mtu kupata UKIMWI.

Je, ugonjwa wa kaswende huambukizwa kwa njia gani?


Kama tulivyosema awali, kaswende husababishwa na bakteria aina ya Treponema pallidum. Miongoni mwa njia za ugonjwa huu nipamoja na ·

Kupitia kujamiiana bila kutumia kinga au ngono zembe na mtu aliyeambukizwa kaswende.

· Mama aliyepata ugonjwa wa kaswende wakati wa ujauzito anaweza kumuambukiza mtoto wake wakati wa ujauzito.

· Kuambukizwa kupitia michibuko au mipasuko kwenye ngozi wakati wa kujamiiana au wakati mwingine pale mtu anapogusana na mtu mwenye kaswende ikiwa wote wawili wana mipasuko kwenye sehemu mbalimbali za ngozi zao.

Sio rahisi mtu kutambua kama ana michibuko au la kwenye ngozi kwani mingine huwa midogo sana isipokuwa ile inayoweza kuonekana kwa macho, lakini huweza kuwa njia ya maambukizo.

Dalili na viashiria vya tatizo hili


Dalili na viashiria vya ugonjwa wa kaswende hutegemea aina ya ugonjwa wa kaswende wenyewe. Kuna aina tano za ugonjwa wa kaswende ambazo ni;

Ugonjwa wa kaswende wa awali (Primary syphilis), Ugonjwa wa kaswende wa pili (Secondary syphillis),  Kaswende iliyojificha (Latent syphilis), Kaswende ya baadaye (Tertiary syphilis. Itaendelea..............

0

Monday, August 8, 2016


Licha ya ladha yake kuwa chungu, mmea wa “Aloe Vera” una faida nyingi kiafya ukitumika kama tiba katika mwili wa binadamu.

Mmea huu umekuwa na majina tofauti tofauti kama ifuatavyo; kwa lugha ya Kiswahili mmea huu huitwa shubiri mwitu, ambapo katika makabila kadhaa mmea huu huitwa majina mbalimbali kulingana na kabila husika.

Wanyaturu huuita ‘mkankiruni’, Wagogo huuita ‘itembwe’ na wahehe huuita ‘Litembwetembwe.’ Mmea huu huwa na umbo linalofanana na mmea wa mkonge au mmea wa mnanasi, ila huu huwa mlaini zaidi.

Majani ya mmea huu yana sehemu mbili, kuna ganda la nje na majimaji ya ndani (jelly). Ganda la nje lina kemikali za kutibu na ule ute wa ndani na lina virutubisho vingi ambavyo husaidia katika kurutubisha kinga za mwili wa binadamu.

Licha ya mmea huu kuwa maarufu duniani kote, umekua ukitumika kama tiba ya magonjwa mbalimbali kwa binadamu na mifugo.

Mshubiri pori umekua ukitumika pia kwa kutengenezea vipodozi vya aina mbalimbali kwa ajili ya masuala ya urembo. Mmea huu hupatikana sehemu nyingi sana duniani hasa katika nchi zenye joto.

Tafiti zilizofanywa na mtandao wa ‘Mediclinic’ kuhusiana na mmea huu, zinaeleza kuwa mmea huu una uwezo wa kuchochea utengenezwaji wa tishu zenye afya katika mwili wa binadamu.

Imebainika pia kuwa mshubiri huo una uwezo mkubwa wa kufanya mfumo wa fahamu kufanya kazi vizuri na kutuliza matatizo yanayoathiri mfumo wa fahamu.

Mbali na hayo, lakini pia mshubiri “Aloe Vera” ukitumiwa kama tiba husaidia kuondoa sumu mwilini. Mmea huu mara nyingi hutumiwa na kina baba kutibu maradhi ya ngiri (Hernia). Kwa hakika mmea huu una maajabu mengi katika suala zima la tiba.

Naweza nikadiriki kusema, mmea huu ni tunu tuliyotunukiwa wanadamu kutoka kwa Mola wetu kwa ajili ya tiba. Sidhani kama kuna mmea wenye uwezo wa kutibu maradhi mengi namna hii kama ilivyo kwa mshubiri pori.

Haijaishia hapo pia, mshubiri hutumika katika kusaidia kujenga seli mpya katika mwili wa binadamu baada ya kupata majeraha kama vile kujikata, michubuko, majeraha ya moto na hata vidonda vya tumbo.

Aidha, husaidia matatizo ya kutopata haja kubwa, maumivu wakati wa haja kubwa na ndogo na hata husaidia kutibu matatizo ya ngozi na chunusi.

Mshubiri umekuwa ukitumika kwa wagonjwa wenye upungufu wa kinga mwilini (UKIMWI) kwa ajili ya kuongeza kinga za mwili (CD4), na imebainika mmea huu unapotumiwa vizuri, mgonjwa wa UKIMWI hujikuta katika hali nzuri.

Watu wengi wamekuwa wakitumia mmea huu kama tiba ya ugonjwa wa malaria, lakini pia mmea huu umekuwa ukichanganywa katika vipodozi mbalimbali ili kuvipa uwezo maradufu wa kutunza ngozi.

Unaweza kutumia mmea huu kwa kukata majani yake na kuyasaga kwa kutumia ‘blender’au kuyatwanga kwenye kinu, na kisha kuyachanganya na maji ya vuguvugu Chuja maji hayo na ongeza maji mpaka upate maji ya kiasi cha jagi moja.

Kunywa vikombe viwili mpaka vitatu kwa siku, kwa muda wa siku tano mpaka saba. Hii itakusaidia kuongeza kinga ya mwili wako na unaweza kurudia dozi hii kila baada ya miezi mitatu mpaka minne.

Ni vema kutumia tiba za mimea ili kuepuka kemikali zisizo za lazima katika miili yetu kiafya. Tukiangalia, pia tunaweza kuona kuwa hata baadhi ya dawa za hospitalini hutengenezwa kwa kutumia mitishamba na mimea ya asili.

Mbali na mmea wa mshubiri kutumika kama tiba kwa binadamu, mmea huu pia unaweza kutumika kama tiba kwa mifugo kama vile kuku. Kwa mfano, ugonjwa wa vidonda vya kuku ambao kwa kitaalam huitwa ‘coccidiosis’ na ugonjwa wa mdondo ambao pia kitaalam hufahamika kama ‘Newcastle disease’ Hutibka kwa kutumia mshubiri.

Baadhi ya watu wamekuwa wakiipanda mimea hii katika bustani za maua majumbani mwao, bila ya kujua umuhimu, faida na maajabu ya mmea huu.

Ningependa kutoa wito kwa Watanzania kutopuuza matumizi ya mmea huu. Ni vema tukautumia kwa ajili ya kinga na tiba za magonjwa mbalimbli katika miili yetu.
5

Saturday, August 6, 2016


Nini maana kukojoa kitandani?

Hii ni hali ya kukojoa kitandani wakati mtu amelala, tatizo hili linapotokea kwa mtoto wa chini ya miaka sita sio ugonjwa na mara nyingi huisha lenyewe.

Watoto wengine huendelea kukojoa kitandani mpaka umri wa kubalehe na kuvunja ungo. Lakini tatizo hili hupotea anapokua mtu mzima kabisa.

Sababu kwanini mtoto anayeweza kukojoa mwenyewe mchana kuendelea kukojoa wakati amesinzia haileweki , mara nyingi watoto wa kiume hujikojolea sana kuliko wa kike lakini kuna mahusiano ya kurithi tatizo hili yaani kuna uwezekano mkubwa baba wa mtoto au mama alikuaga kikojozi pia kwenye utoto wake.

Kwa watu wazima tatizo la kukojoa kitandani hua ni ugonjwa flani. Mfano wa magonjwa haya ni,

Kisukari (diabetes mellitus):

Ugonjwa huu huambatana na dalili ya kupata kiu sana, njaa kali na kwenda kukojoa mara kwa mara wakati wa usiku.

Magonjwa ya njia ya mkojo (chronic urinary tract infection):
Hii ni kutokana na kuharibika kwa kibofu cha mkojo ambacho ni muhimu katika kutambua ujazo wa flani wa mkojo ili mtu aende kukojoa hivyo kuugua kwa kibofu husababisha kisifanye kazi vizuri. mfano cystitis

Magonjwa au kuumia kwa mishipa ya fahamu ( structural or infections of nerves):

Mishipa ya fahamu ni muhimu katika kutoa taarifa za ujazo wa mkojo kwenye kibofu. Kibofu kinapofikisha ujazo wa 300mils mpaka 400mils taarifa hutumwa kwenye ubongo, kisha ubongo hurudisha taarifa za kuruhusu mtu akojoe.

Kuharibika kwa mishipa hii ya fahamu husababisha kujikojolea mfano kuvunjika kiuno, kiharusi, magojwa ya akili, multiple sclerosis na alzeheimers disease.

Kuvimba kwa tezi dume (prostate enlargement):

Tezi dume ni kiungo kinachopitiwa katikati na mirija ya mkojo{urethra}, hivyo kuvimba kwake hubana mirija hiyo na kusababisha kukojoa mara kwa mara[incontinence}.

Vipimo ambavyo hupimwa mahospitalini:

Kupima mkojo kuangalia kama kuna shida yeyote ya mfumo huo.

Kupima puru kama tezi dume imevimba.{digital rectal examination}

X-ray kuangalia kama kuna tatizo la umbo la kibofu cha mkojo.

Kama Unasumbuliwa Na Tatizo Hili Fika Leo Afya Bora Herbal Clinic Iliyopo Njia Panda Ya Kigogo, Karibu na Roundabout kupata tiba na tatizo kutojirudia tena.
0


Inaweza ikawa ndoto yako ni kupata motto wa kiume lakini kila unapojifungua hubahatiki kumpata ukweli ni kwamba kila jambo linapngwa na si kutokea kama miujiza.

Ukweli ni kwamba unaweza mpata motto wa jinsi yoyote unayohitaji iwe wa kiume au au wa kike na hata mapacha.

Inafahamika kwamba watu wengi wamekua wakitamani jinsia flani za watoto ili wazae watoto wachache ila kukosa jinsia waliyoipanga hujikuta wakizaa watoto wengi wakati wakitafuta jinsia husika, mpaka familia hugombana na kutengana kwa sababu hizi.

Mara nyingi wazazi wa kiume hufikia hatua ya kuvunja ndoa kabisa hasa wanapokosa watoto wa kiume.

Leo nitamaliza kitendawili hiki kwa kutoa njia ambazo zinaweza kufanya mtu kupata mtoto wa kiume kwa asilimia nyingi…

Kitaalam mbegu zinazotoa mtoto wa kiume XY huenda kwa mwendo mkali sana kwenda kwenye mfuko wa uzazi lakini hufa haraka lakini mbegu zinazotoa mtoto wa kike XX husafiri taratibu na huchelewa kufika na kufa ndani ya mfuko wa uzazi kwani mbegu hizi huweza kuvumilia hali mbaya ya kimazingira ndani ya mfuko wa uzazi wa mwanamke.

Hivyo njia pekee ya kupata mtoto wa kiume ni kuhakikisha mbegu hizo za kiume XY zinakutana na mayai ya kike kwenye mfuko wa uzazi haraka kabla ya kufa..

Usipate taabu tena na kutotimiza malengo au ndoto yako ya muda mrefu, fanya mambo haya ili upate motto wa kiume:-

Hakikisha unashiriki tendo la ndoa siku mayai ya mwanamke yanapokua yameshuka (ovulation).

Ukishiriki tendo la ndoa siku hii ambayo yai linakua limeshuka mbegu za kiume huweza kufika mapema na kujiunga na mayai ya kike na kutengeneza motto (fertilization) hii ni siku ya 14 kabla ya kuona damu ya mwezi unaofuata sio baada ya kuona siku zako..

Kama wewe mwanamke hujui siku yako ya ovulation fanya hivi.


Pima joto lako la mwili: nunua kipima joto[thermometer} na kisha pima joto lako kila asubuhi ,  siku ukiona joto lako limeongezeka kidogo ujue umeanza ovulation na hiyo ndio siku muhimu ya kutafuta mtoto..

Angalia maji maji ya uke: kawaida maji ya uke hua mazito na kuvutika kama maji ya mayai mabichi wakati mwanamke anapoanza ovulation..

Wewe mwanaume ongeza idadi ya mbegu zako (sperm count)

Mwanaume anatakiwa aongeze wingi wa mbegu zake hasa kwa kukaa siku mbili mpaka tano bila kushiriki tendo la ndoa wakati akisubiri mwanamke wake aanze ovulation.

Njia zingine za kuongeza mbegu ni:
Weka korodani kwenye hali ya ubaridi: kawaida korodani hutengeneza mbegu nyingi wakati wa hali ya ubaridi kuliko joto hivyo mwanaume anatakiwa kuepuka kuvaa nguo zilizobana sana, na kuweka laptopkwenye mapaja

Acha kuvuta sigara na kunywa pombe: wanaume wanaokunywa pombe na kuvuta sigara hua na mbegu kidogo sawasawa na wavutaji wa bangi..

Matumizi ya dawa za cancer pia husababisha uzalishaji wa mbegu kidogo sana.

Tumia style za ngono ambazo zinahamasisha muingilio mkubwa (deep penetration)

Hii huzipa faida mbegu za mtoto wa kiume (XY) kufika haraka na kufanya fertilization na upande mwingine, muingiliano mdogo (shallow penetration) husababisha mbegu kumwagwa mbali na mlango wa mfuko wa uzazi hivyo mbegu huweza kukutana na hali ya tindikali kwenye uke hivyo mbegu za mtoto wa kiume kufa haraka na kuziacha mbegu zinazotoa mtoto wa kike ( XX).

Hakikisha mwanamke anafika kileleni:


Mwanamke anapofika kileleni hutoa maji mengi ukeni ambayo hupunguza wingi wa tindikali ambayo ni adui wa mbegu zote hasa mbegu za mtoto wa kiume XY ambazo hua haziwezi kuvumilia hali ngumu ya kimazingira.

Usifanye tendo la ndoa kabla na baada ya ovulation


Kabla ya ovulation mbegu za mtoto wa kiume XY hufika haraka kwenye mfuko wa uzazi kama kawaida na kukuta mayai ya mwanamke hayajafika na kufa vivo hivyo baada ya ovulation..kwa maelezo zaidi soma hapa.

Je, Unasumbuliwa Na Matatizo Ya Uzazi Na Haupati Mtoto, Fika Leo Afya Bora Herbal Clinic Iliyopo Njia Panda Ya Kigogo Karibu na Roundabout kupata tiba ya tatizo hilo.
0


Huenda ukawa unataabika kila siku hujapata motto hata mmoja kutokana na kutofahamu kwa namna gani au ni siku ipi ambayo ukishiriki tendo la ndo utapata mimba. Kwani kila hupangwa hakitokei tu kama miujiza.

Siku za hatari za mwanamke ni zipi?
Hizi ni siku ambazo mwanamke akishiriki ngono bila kutumia kinga anapata ujauzito bila wasiwasi wowote labda kama ana matatizo yanayomfanya asibebe mimba au mwanaume wake ana matatizo.

Utazijuaje siku hizo?
Kwanza kabisa ili ujue siku zako za hatari lazima ujue idadi ya siku za mzunguko wako. Kuna aina tatu za mzunguko.. mzunguko mrefu ambao unachukua siku 35, mzunguko mfupi unaochukua siku 25 na ule wa kawaida unaochukua siku 28 na ndio mzunguko ambao watu wengi wanao.

Unajuaje mzunguko wako?
Hesabu siku tangu siku ile ya kwanza uliyoona siku zako za hedhi mpaka siku moja kabla ya kuona siku zako za hedhi zinazofuata. Unashauriwa uchukue miezi mitatu mpaka sita ukihesabu ili ue na uhakika kwamba mzunguko wa tarehe zako haubadiliki, kama umeshahesabu siku za nyuma kabla ya kusoma makala hii ni vizuri pia. Mfano umeanza kuona siku zako tarehe moja mwezi wa nne alafu ziko zako zingine ukaziona tarehe 29 mwezi wa nne, chukua 29 toa 1 utapata 28.. maana yake wewe unamzunguko wa siku 28.

Je siku za hatari ni zipi?

siku ya hatari ni siku ya 14 kabla ya kuona hedhi inayofuata na sio siku ya 14 baada ya kuona hedhi iliyopita na hapa ndio watu wengi wanachanganya na kupata mimba.

Mfano kama mzunguko wako ni siku wa kawaida siku 28, chukua 28 toa 14 utapata 14. Hivyo siku yako ya hatari ni siku ya 14, lakini kwa kua mbegu ya kiume inaweza kuishi mpaka siku tano na yai la kike linaweza kuishi mpaka masaa 24 ndani ya mfuko wa uzazi basi siku nne kabla na siku moja baada ya siku ya 14 ni hatari hivyo siku za hatari ni ni siku ya 10,11,12,13,14 na 15.

Kama mzunguko wako ni mrefu labda siku 36 basi chukua 36 toa 14 utapata 22. Hivyo siku ya 22 ni hatari na zingine ni 18,19,20,21,22 na 23.

Kama mzunguko wako ni mfupi, mfano mzunguko wa siku 21, sasa ukichukua 21 ukatoa 14 unapata 7 yaani siku ya saba ni hatari kwa huyu mtu.hivyo siku zingine za hatari ni 3,4,5,6,7[mtoto wa kiume] na 8.

Dalili kwamba uko kwenye siku za hatari ni zipi?

Kuongezeka kwa joto kidogo, tumbo kuuma kidogo, na ute mweupe kutoka sehemu za siri..

Maelezo hayo hapo juu yanaweza kusaidia kupanga uzazi, kuchagua jinsia ya mtoto au kutafuta mtoto. Lakini pia tarehe zote nilizoweka mabano ambazo ndio tarehe yai linashuka ndio za mtoto wa kiume zingine zote zilizobaki ni za watoto wa kike.

Fika Leo Afya Bora Herbal Clinic Iliyopo Nji Panda ya Kigogo Karibu na Roundabout Kama Una Tatizo la Ugumba Uweze Kutibiwa na Kupata Mtoto.

0

ANDIKA MAONI YAKO

Name

Email *

Message *